Posts

Showing posts from April, 2020
Image
TUMAINI KATIKA UPEO WA MACHO Biblia imejaa matumaini. Mtume Paulo hasa ni mtume wa matumaini. Anaandika kwa kanisa la Rumi, anawatia moyo kwa maneno haya, "kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kwa saburi na faraja  ya maandiko tupate kuwa na tumaini" Warumi 15:4. Sura ya 15 inahitimisha na maneno haya: " Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu". Wakati siku zijazo zinapoonekana kuwa na mashaka, Neno la Mungu hujaza mioyo yetu kwa tumaini. Paulo akimwandikia Tito katika Tito 2:13 anamthibitishia kudumu " ukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na mwokozi wetu. Historia ilikuwa na mahali pa kuanzia na itakuwa na mahali pa kuishia. Ilianza Mungu alipoimba dunia hii, na upeo wa uumbaji ni kurudi kwa Bwana wetu, ambaye hatimaye ataumba upya mbingu mpya na nchi mpya. Kuna m...
WAKATI TAABU ITAKAPOKOMA Bwana Yesu asifiwe Sana...! Tunapoendelea na juma la maombi kupitia Idara ya Uchapishaji...  Tunakumbushwa kwamba tunapaswa kutumika shambani mwa Bwana kwa kujitoa kikamilifu kufanya kazi ya Mungu aliyotutuma tufanye katika Mathayo 28:18-20 Mungu anatuhitaji tuwafundishe wenzetu habari njema ya wokovu wetu. Hivyo, Kupitia juma hili tunakumbushwa kugawa kitabu cha WAKATI TAABU ITAKAPOKOMA. Kitabu hiki kinauzwa Tsh. 2,500/- tu. Nikusihi muumini mwenzangu kwa moyo mkunjufu, hebu jitoe, na umwombe Mungu akusaidie ili ugawe kitabu hiki. Kwa maelekezo zaidi tumia namba hizi +255683645322 Mungu akubariki sana unapojitoa.
Image
VITABU  MUHIMU VYA KUSOMA kwa wakati Kama huu usipoteze fedha na muda kusoma udaku , kuna vitabu vya muhimu kusomwa na kila Mtu katika ulimwengu wetu. Ikiwa ni juma la maombi kupitia Idara ya Uchapishaji; Hebu na uchukue hatua ya kusoma na kugawa angalau kitabu kimoja kwa ajili ya rafiki yako. 1) PAMBANO KUUU - kitabu hiki kinaelezea  PAMBANO KUU katika ya wema na uovu kwa uwazi KABISAA,kinaelezea pambano lolilopo katika Kristo na shetani na mawakala wake ,kinaelezea Maendeleo ya pambano kati ya KWELI NA UDANDANYIFU  ,kinaelezea Vita KUU kati ya BIBLIA NA MAPOKEA KWA UWAZI ..hiki ni kitabu kinachofuatia Biblia kwa Ubora ,ukitoa Biblia kitabu hiki kinashika nafasi ya KWANZA 2) MATUKIO YA SIKU ZA MWISHO -kitabu kinaelezea yanayoendeelea kutokea katika ulimwengu wa leo mpaka Mwisho wa wakati 3) WAZEE NA MANABII 4) MANABII NA WAFALME 5) TUMAINI LA VIZAZI VYOTE 6) DHIKI KUU INAKUJA LAKINI KUNA TUMAINI 7) KITABU CHA DANIELI 8) KITABU CHA UFUNUO 9) taja kitab...
Image
SAFINA NDANI YA SAFINA YA KWELI. Na. Mch Filbert Joseph Mwanga Fungu kuu: Mwanzo 6:14 Wimbo No: 107 Kanisa la Mungu ndiyo SAFINA ya hapa duniani inayotuongoza kuifikia SAFINA ya kweli ya mbinguni. Ndani ya Kanisa lipo Idara ya Shule ya Sabato ambayo ndio Moyo wa kanisa unaodunda barabara. Tusiposimamia Idara hii vyema basi haitadunda barabara. Mwanzo wa machukizo yalianza kipindi cha Nuhu wakati wana wa Mungu walipo anza kwenda kinyume na mapenzi ya  Mungu. Mwanzo 6:1,2...inaelezea Ndoa za mseto zikaongezeka, kilikuwa kipindi cha uasi, hawakujua kuwa Mungu ndiye aliwaumba. Wana wa Mungu ni wale pekee wanaomtii Mungu kupitia sheria zake. Kumbukumbu la Torati 14:1... Inaelezea zaidi juu ya wana wa Mungu. Yohana 1: 12; inasema wote waliompokea Bwana (Yesu Kristo) yeye huyo Yesu aliwafanya kuwa watoto wa Mungu. Kaini baada ya kufanya dhambi ya kumuua ndugu yake (Habili) watoto wake hawakuitwa Shetani bali ndio tunaambiwa katika kitabu cha Mwanzo 6: 1,2 kuwa ni wana wa ...